Page 30
Ni Kanuni
“Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili awake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho” [Wagalatia 6:7-9].
Mungu aliziandaa kanuni za kiroho, kama alivyoziandaa kanuni za asili, ili kukidhi makusudi ya uumbaji wake. Ujinga ya kanuni haiizuii kutenda kazi. Kama mtu ataruka kutoka ghorofa ya hamsini bila kujua kanuni ya uvutano, lazima wataanguka. Huu ndiyo ukweli kwa mtu
anayeangamia kwa kukosa maarifa [Hosea 4:6].
Kwa njia hiyo, kila siku huwa tunatembea katika matokeo ya kanuni za kiroho hata kama hatujui jinsi zinavyofanya kazi. Moja ya kanuni hizi ile ya kupanda na kuvuna. Kanuni hii inasema kwamba tutavuna kile mavuno. Ni dhahiri. [Wagalatia 6:7-9] Na mavuno yatakuwa ni matokeo ya kile tulichopanda. Haijalishi kama tunajua kuwa tunapanda au la! Kwa namna yo yote ile – zao litafikia wakati wa kuvunwa.
Tunazipata wapi mbegu tunazopanda?
Kumbukumbu la Torati 30:19-20 inasema, “Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chaguauzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako.”
Kuna magunia mawili ambamo mbegu zinaweza kutolewa— gunia la maisha na gunia la kifo. Kila kitu kinachopandwa hutoka katika moja ya magunia haya. [Yohana 10:10] Hakuna mbegu za katikati.
Yesu husia mbegu kutoka kwenye gunia la uzima. Shetani husia mbegu kutoka kwenye gunia la mauti. Tunapookolewa tunaanza kuchagua mbegu inayoleta uzima, [Warumi 8:5,6] lakini kwa bahati mbaya tabia zetu za zamani hufa pole pole.
Mbegu zinazopandwa zinaweza kuwa ni maneno, nia au matendo. Kupanda ni mchakato endelevu. Ni muhimu sana kutumia mbegu sahihi. Unapaswa kutambua unapanda nini. Mbegu tunazochagua hupandwa maishani—maisha yetu, maisha ya wenzi wetu, watoto wetu, na wengine.
Moyo ni udongo ambapo mbegu hizi huotesha mizizi na kukua [Yeremia 4:3,4]. Kutokana na Mathayo 13:18-23, kuna aina mbalimbali za udongo.
Udongo wa mawe na miiba hufanya mbegu ziote kwa shida hivyo kutopata mazao yenye afya.
Udongo ambao tunapanda mbegu lazima umwagiliwe kwa neno la Mungu, ili kuupa afya ili uzae matunda mengi. Udongo uliomwagiliwa vizuri kwa neno la Mungu hausaidii tu kupata mazao mengi, bali pia hurahisisha kazi ya kuondoa magugu.
Yeremia 4:3 inasema kuulima udongo katika konde zetu (ardhi ambayo haijalimwa). Hii inaashiria moyo kadiri tunavyojiandaa kuipokea mbegu ya Mungu.
Ndani ya mioyo yetu, tunatifua udongo ambao haujalimwa bado kwa maombi mengi na kwa kutumia muda mwingi kusoma neno la Mungu. Kama tukiomba kwa ajili ya moyo wa mtu mwingine ili uandaliwe, tunaomba na kupigana vita vya kiroho.
.
Maingiliano
Kwa kutambua kwamba mbegu unazopanda ni maneno, mitazamo na matendo.
Chukua dakika chache na zingatia mbegu moja nzuri ambayo kila mmoja amepanda katika eneo lolote kati ya haya.
Page 31 © 2=1 ~ Gundua Nguvu
Mambo ya Mavuno
- Mavuno huja kwa majira tofauti nay ale ya upandaji. Hakuna mkulima ambaye huvuna mara baada ya kupanda. Baada ya kuwa umeuandaa udongo wako na kupanda mbengu, endelea kumwagilia maji ya neno la Mungu. Tia mbolea ya matendo yako [Yakobo 2:26]. Usiichimbue mbegu yako ili kuona kama inaendelea vizuri na kuvuna mavuno ya yasiyokomaa kabla ya majira yake kwa sababu una haraka ya kuona matokeo. Zao lako litakapoonekana halitaonekana kama ulivyolipanda [Marko 4:26-29]. Pale mkulima anapopanda mahindi, kile kimmea cha kijani kinachoanza kuchipuka huwa hakifanani na gunzi lililosheheni punje za mahindi. Usikate tamaa na kuliharibu zao lako. Lipe muda wa kukua.
- Utavuna kile ulichopanda. Wagalatia 6:7 Biblia yenye tafsiri ya NENO inasema, “Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna.” Hakuna mkulima aliyepanda mahindi akatarajia kuvuma ngano. Ndivyo ilivyo, ukipanda upendo ni hakika kuwa utavuna upendo.
- Mara zote utazalisha zaidi ya kile ulichopanda [Hosea 8:7; Mathayo 13:8]. Kwa kila mbegu unayoipanda, zao litakapotokea litakuwa limesheheni aina ile ile ya mbengu. Gunzi moja la mahindi litazalisha mamia ya mbegu, kama siyo maelfu, ya magunzi ya mahindi. Kama mbegu hizi mpya zikapandwa zitaendeleza mazao ya hapo baadaye yakiwa ya aina ile ile, lakini kwa kiasi kingi zaidi. Kanuni hizi za kupanda na kuvuna zinarahisisha kuona katika ndoa zetu jinsi ambavyo ndoa zetu zimeendelea kudidimia kwa muda wa miaka mingi iliyopita.
Wengi wamepanda kifo kwa ujinga wao—na kuvuna mazo ya—mbegu ile ile na— kuvuna uharibifu mkuu.
Page 32 © 2=1 ~ Gundua Nguvu
Mambo ambayo yalikuwa ni maudhi madogo madogo yamefanyika kuwa maeneo makubwa ya ugomvi.
Adui amefanya juhudi ya kutuletea mbegu za mauti na tumekuwa tukizipokea. Tangu leo, anza kuchagua mbegu ziletazo tabia inayoimarisha uhai. Kusudia moyoni mwako kuzipalilia ili upate mazao mengi.
Kadiri tunavyotambua kile tutakachokivuna, ni muhimu pia kutambua aina ya mazao mema tuliyokwisha kuyazalisha. Kuna uwezekano wa kulenga mazao yasiyofaa. Umepata mbegu njema pia. Gundua aina ya mbegu ulizopanda ili kuzalisha mazao mema na uchague mbegu zile zile ili uendelee kuzalisha mazao hayo.
Chunga usije ukaangukia kwenye mashutumu ya mazao hafifu. Badala yake, tubu. Toba ni kama dawa inayoua magugu shambani iliyopulizwa kwenye mazao hayo hafifu. Huanza kufa mara moja, lakini inaweza kuchukua muda kabla hayajafa kabisa. Ni kweli, mazao hayo hafifu wakati mwingine huonekana kuanza kwa kupata changamoto ya ukuaji. Usikate tamaa. Hatimaye, mazao yasiyofaa huondolewa na kurudishiwa mbegu bora inayotokana na mazao bora yanayoendelea vizuri.
Usipokee mashutumu kutoka kwa adui. Mungu atarejesha na kuboresha maeneo ambayo yameota mazao yaliyo hafifu [Joeli 2:25]. Kadiri unavyotubu na kupanda mbegu njema, inaweza kuchukua muda mrefu kidogo kabla ya kuvuna. Usikate tamaa! Kama utajikuta unapanda isivyo tena, uwe mwepesi wa kutubu [1 Yohana 1:9; Kumb. 22:9]. Zao lile za zamani lazima life. Anza kuchagua mbegu za kupanda kutoka kwenye mfuko wa Mungu wenye mbegu.
Fuata Kumbukumbu la Torati 30:19. Chagua kupanda Neno na tabia za kitauwa. Mwombe Mungu akupatie mbegu za kupanda [2 Wakorintho 9:10].
Andaa udongo wako vizuri [Yeremia 4:3]. Kwa ajili ya moyo wako, pata muda wa kuomba na kusoma neno la Mungu. Unapanda ndani ya mtu mwingine, pata muda wa kutosha katika maombezi na vita vya kiroho.
Sema Neno na kulipanda. Hata Mungu hulisema neno lake na kuona vitu vinapita [Mwanzo 1:3,6,9,11; Isaya 55:11]. Rutubisha mbegu yako kwa matendo inayofaa kwa mavuno unayoamini kuwa utayapata [Yakobo 2:26].
Kulingana na 2 Wakorintho 10:5, Shetani anatafuta kupanda mbegu zake mawazoni mwako. Angusha kila wazo baya. Waza juu ya mambo ambayo Bwana ametuamuru katika Wafilipi 4:8. Usipokee mbegu ya adui.
Mapigano
Yakobo 3:16 inasema, “Maana palipo na wivu na ugomvi, ndipo palipo na machafuko na , na tendo baya.” Mithali 20:3a inasema, “Mtu kujitenga na ugomvi ni heshima kwake.” Kwa kuchunguza madhara ya ugomvi, wanandoa wasiruhusu kabisa katika nyumba yao.
Ugomvi ni kama moto. Mtu mmoja akiuwasha baadaye huzimika wenyewe. Lakini kama mtu mwingine atatia mafuta ya taa, moto huo utawaka zaidi. Na inakuwa vigumu kuuzima. Na kama mtu mwingine naye ataongeza mafuta ya taa, basi utaongezeka zaidi na inakuwa ni vigumu zaidi kuuzima [Mithali 15:1]. Jawabu hapa ni kusitisha ugomvi mara pale unapoanza.
Ni muhimu kuzuia ugomvi kuliko kuhihesabia haki [Mathayo 23:12].
Kumbuka, mwenzi wako siyo adui yako, ni Shetani [Waefeso 6:12].
Panda upendo, amani, na utulivu pale unapomwona mwenzi wako akipanda ugomvi [Warumi 12:21; Wafilipi 3; Wagalatia 5:14,15].
Page 33 © 2=1 ~ Gundua Nguvu
Hakika mazao ya kile ulichopanda na kwa kiasi kikubwa [Wagalatia 6:7-9]. Hapatakuwa na mapigano au ugomvi kama mtu wa pili hatakuwa tayari kuichochea hali hiyo.
Fanya vivyo hivyo hata kwa watoto wako. Panda upendo pale wanapopanda ugomvi. Funga kazi ya yule mwovu, bali mpende mwanao kweli kweli.
Kuna uwezekano mdogo sana kwamba mfumo wa ugomvi unaweza kuvunjwa kwa nguvu za kimwili. Inahitaji nguvu za Mungu ili kuleta mabadiliko. Njia moja nzuri ya kupinga ugomvi ni kuvunja ugomvi huo.
Kila mwenzi anapaswa kumruhusu mwenzake kuita nguvu ya kuvunja ugomvi wakati wo wote yanapojitokeza kati yao. Kuita nguvu ya kuvunja ugomvi ni kukubali kwamba wote wawili mko katika ugomvi. Huchukua watu wawili ili kuleta ugomvi. Usiseme, “Wewe ndiye unayesababisha ugomvi,” au “Ni wazi kwamba wewe ni mgomvi.”
Kila mmoja wenu anapaswa kusema, “tunahitaji nguvu ya kuvunja ugomvi!”
Kisha ninyi wawili mnakubaliana na kile Roho anachokisema [Yakobo 3:3-10]. Kama umebatizwa katika Roho Mtakatifu, tunawashauri mwombe au msali pamoja katika Roho kwa muda wa dakika tatu. Kama mtajaribu kurefusha muda huo, baadaye hamtakuwa na hamu ya kuendelea na zoezi hilo. Kama mtajaribu kufupisha zaidi, yawezekana haitakuwa na manufaa yo yote.
Kama hamna mazoea ya kuomba katika Roho, tutakuwa tukijifunza juu ya Ubatizo wa Roho Mtakatifu katika Juma la Saba.
Kama ugomvi ndiyo tatizo la mahusiano yaenu na msingependa kusubiri mpaka Juma hilo la Saba, tafadhali onana nasi baada ya kipindi.
Kwa kuomba katika Roho, utakuwa unapanda katika Roho na siyo katika mwili [Wagalaatia 6:8],
Na kujenga umoja katika mahusiano yenu. Mazao yatatokana na kile ulichokipanda
Page 34 © 2=1 ~ Gundua Nguvu
MAELEZO YA MAJADILIANO
© 2=1 ~ Gundua Nguvu
Nguvu ya Kupanda na Kuvuna Wiki 4
Msidanganyike: Mungu hawezi kudhihakiwa. Mtu huvuna alichopanda. Wagalatia 6:7
Kwa nini kutoamini jambo hili kumdhihaki Mungu?
Je, andiko hili linaweka mipaka yoyote juu ya aina gani ya kupanda au lini au wapi?
Je, hii ina maana gani kwako binafsi kwa maisha yako ya kila siku?
Tusichoke katika kutenda mema, maana tutavuna kwa wakati wake tusipozimia roho. Wagalatia 6:9
Kwa nini tunakuwa “tukichoka katika kutenda mema” ikiwa hatuoni matokeo mara moja?
Unafikiri ni nini huamua “wakati ufaao”?
Unafikiri kukata tamaa kunaonekanaje?
Leo ninaziita mbingu na ardhi kuwa mashahidi dhidi yenu, kwamba nimeweka mbele yenu uzima na kifo, baraka na laana; sasa chagua uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi. Kumbukumbu la Torati 30:19
Unafikiri kwa nini Mungu anatupa uchaguzi?
Kwa nini Mungu ana mbingu na dunia kuwa mashahidi?
Maandiko haya yanasema nini kuhusu matokeo ya kizazi cha chaguo zetu?
Kwa wale waishio kama ubinadamu wao huwaambia watawale akili zao kwa yale asili ya kibinadamu inataka. Wale wanaoishi kama Roho anawaambia wadhibiti nia zao kwa yale Roho anataka. Warumi 8:5
Angalia andiko hili halisemi “kushawishiwa” bali linatumia neno “kudhibitiwa”. Hiyo inakuambia nini?
Unawezaje kubadilisha kile kinachokudhibiti?
Sasa basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Warumi 8:1
Tunasikia sehemu ya kwanza ya andiko hili ikinukuliwa mara nyingi, lakini nusu ya pili inasema nini kuhusu kuwa huru kutokana na hukumu?
Mara nyingi tunasikia watu wakisema kwamba mtu fulani anawawekea hukumu. Andiko hili linasema nini kuhusu hilo?
Ikiwa tunahalalisha jambo fulani maishani mwetu ambalo andiko linatuambia kuwa ni dhambi na hata tunasisitiza kwamba ni Mungu aliyetuambia tufanye hivyo, je, tutapambana na hukumu? Kwa nini au kwa nini?
Palipo na husuda na ugomvi, pana machafuko na kila kazi mbaya. Yakobo 3:16
Kwa nini unafikiri ugomvi ni mlango wa kila kazi mbaya?
Mara tu maneno yanaposemwa, yapo nje na hayawezi kurejeshwa. Walianza mwendo zaidi sana. Tunawezaje kushughulika na maneno yetu tunaposema jambo ambalo linaumiza wenzi wetu?
Kuanzia sasa utumie Mapumziko ya Ugomvi wakati kuna ugomvi kati yenu? (Dakika tatu kuomba katika roho)
Sasa yeye ampaye mpandaji mbegu na mkate kwa chakula atawapa na kuongeza akiba ya mbegu zenu na atazidisha mavuno ya haki yenu. 2 Wakorintho 9:10
Je, tunahitaji kuogopa kwamba tunaweza kupanda sana kitu kizuri?
Ikiwa ndivyo hivyo, kwa nini tunafikiri mambo kama vile “Nimetoa sana” au “Sina upendo zaidi wa kutoa?
Nani anawajibika kuunda mavuno makubwa zaidi?
© 2=1 ~ Gundua Nguvu